MTANGAZAJI

MAHABUSU KADHAA ARUSHA WAGOMA KULA ILI KESI ZAO ZISIKILIZWE



Mahabusu  kadhaa walioko katika gereza kuu  la Arusha wanaotuhumiwa kwa makosa ya kukutwa na madawa ya kulevya aina ya bangi na mirungi imeelezwa kuwa afya zao zimezorota kutokana na kugoma kula chakula kwa kipindi kirefu ili kushinikiza vyombo husika kusikiliza kesi zao.

 Baadhi ya mahabusu hao ambao waliweza kuzungumza na waandishi wa habari  mara baada ya kufikishwa  katika mahakama kuu jijini Arusha jana walieleza kuwa hali hiyo inatokana na kesi zao kukaa kwa muda mrefu bila kusikilizwa,baadhi yao  kesi zikiwa na zaidi ya miaka miwili bila kusikilizwa jambo ambalo limewafanya kuonyesha hisia zao kwa njia ya mgomo wa kula chakula katika kushinikiza vyombo husika kusikiliza kesi zao ili kubaini wana hatia ama la.

 Mwandishi wa habari hii  ilishuhudia mahakamani hapo kwa kuwaona mahabusu hao wakigoma kushuka kutoka kwenye karandinga lililokuwa limewaleta mahakamani hapo.Hata hivyo baada ya muda mrefu baadhi yao walianza kushuka katika basi hilo na hii ni baada ya kubembelezwa kwa muda mrefu.

Baada ya tukio hilo Mwandishi wa habari hizi alimtafuta msajili wa mahakama wa kanda ya kaskazini ndugu Mashauri ambaye hakuwepo mahakamani hapo na alipozungumza kwa simu alisema yuko nje ya mahakama hiyo Karatu kikazi hivyo  hana Taarifa  juu ya mgomo huo  Nakuahidi kufuatilia swala hilo.   


No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.