MTANGAZAJI

MVUA ZAKATA MAWASILIANO KYELA,MBEYA



Mvua kubwa zinazoendelea kunyesha zimekata mawasiliano yanayoziunganisha barabara za Kyela Mjini na Ipinda,Ipyana, Katumbasongwe, Bujombe,Bandari ya Kiwira Kasumulu,Kyela na Ibungu, baada ya  daraja la watembea kwa miguu kusombwa na maji.

Tathmini ya awali iliyotelewa na uongozi wa wilaya kwa  mbunge wa kyela Dk Harrison Mwakyembe inaonesha kuwa kata 11 kati ya 20 za wilaya hiyo,zimeathirika na mafuriko,huku kata mbili za Bujonde na Kajunjumele zikiathirika kwa kiwango kikubwa zaidi.

Mafuriko hayo pia yamesababisha vifo vya watu watatu,huku wengine watatu, hawajulikani waliko,zaidi ya kata 60 hazina makazi baada ya nyumba zao kukumbwa na mafuriko na sasa wamejihifadhi kwenye majengo ya shule zilizosalimika.

Waathirika wa mafuriko hayo wanahitaji msaada wa haraka wa chakula,mavazi na malazi huku Baadhi ya wakazi  wa kyela wanasema kuwa mafuriko hayo ni makubwa kuzidi ya mwaka 1952 na yale ya mwaka 1978.


No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.