MTANGAZAJI

WATEKAJI WATAKA DOLA MILIONI MOJA KWA KILA KICHWA

 


Kikundi cha Wahalifu huko Haiti kimeeleza kuwa kinataka malipo ya Dola milioni moja kwa kila mtu ili kuwaachia Wamishonari na watoto lililowateka.

Waziri wa Sheria Liszt Quitel amethibitisha kwamba matakwa hayo yamepokelewa iikiwa ni masharti ya  kuachiwa kwa watu hao 17 waliotekwa nchini Haiti.

Wamishonari  17 kutoka Marekani na Canada ambao miongoni mwao ni vijana chini ya miaka 18 walitekwa  nchini Haiti asubuhi ya Oktoba 16 mwaka huu.

 Kundi hatari la uhalifu nchini Haiti 400 Mawozo linaaminika kuhusika na utekaji huo kwa mujibu wa duru za mamlaka za usalama za nchi hiyo.
 
 Taarifa ya Mkuu wa Idara ya Habari ya  Ikulu ya Marekani Jen Psaki amesema kuwa Ikulu hiyo na FBI wanafanya jitihada za kuwaokoa mateka hao.

 Kwa mujibu wa taarifa za Kituo cha Utafiti na Uchambuzi wa Haki za Binadamu nchini Haiti (CARCH) takribani matukio 628  ya utekaji 628 yametokea kuanzia Januari, yakihusisha wageni 29,Kundi la 400 Mawozo limedai fidia ya karibu Dola za Kimarekani 20,000. 
 
 

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.