MTANGAZAJI

RIPOTI YAONESHA MGONJWA ALIFARIKI BAADA YA KUWEKEWA DAMU ISIYO YA GROUP LAKE

Ripoti hiyo yenye kurasa 100 imetolewa na Rais wa hospitali hiyo Doug Lawason akieleza kusikitishwa kwake na tukio hilo ambapo amesema kuwa mwanamke aliyepoteza maisha ambaye alikuwa na miaka 75 wakati huo aliwekewa damu ambayo hakupaswa kuwekewa wakati akiwa kitengo cha magonjwa ya dharula hospitalini hapo.

Mwanamke huyo aliyekuwa na damu ya group B+  alifika hospitalini hapo mwanzoni  mwa mwezi Disemba mwaka jana  akiwa na tatizo la kuvujia damu katika ubongo wake kisha akawekewa damu ya group A+ na baada ya hapo akapata shinikizo la damu ndani ya masaa matatu na kisha kupoteza maisha siku iliyofuata.


No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.