MTANGAZAJI

MWIMBAJI WA BASS WA SONDA YA DIHLU FABIAN WEREMA "MR BASS" AJA KIVINGINE (+VIDEO)


Fabian Werema

*Mianzo*
FabianWerema  anaanza kuifahamisha mtangazaji.com kuwa karama ya uimbaji ilikuzwa na mama yake mzazi kupitia Kwaya ya Waadventista ya Kitunda jijini Dar es salaam mwaka 2005 akiwa ni mwimbaji wa sauti ya tatu

Iliopofika mwaka 2012 alihamia  mkoa wa Mara kwa ajili ya masomo katika Shule ya Sekondari ya  Ikizu inayomilikiwa Kanisa la Waadventista wa Sabato nchini Tanzania na hapo akiwa na waimbaji wengine wanne walianzisha kikundi cha uimbaji wa nyimbo za injili kwa mtindo wa Acappella akiwa ni mwimbaji mwongozaji.


Fabian anaeleza kuwa mwaka  2014 alirudi jijini Dar es salaam Dar es salaam na kutafuta kundi la kujiunga nalo katika uimbaji.


"Kuna siku nilikuwa nasikiliza mahojiano kwa Morning Star Radio  ya kikundi cha Sauti ya Matumaini ambacho kwa sasa hakipo, ila nilivutiwa nao na walipotoa mawasiliano nilichukua namba na kuomba kujiunga nao,nilifanikiwa kujiunga kama mwimbaji wa sauti ya pili" anasema Mr Bass

*Kutoka Sauti ya 3,1,4 hadi Bass* 

" Siku  moja nilikuwa najaribu kuimba wimbo wa Sonda ya Dihlu nikiwa na kundi la Sauti ya Matumaini kwa sababu Sabato hiyo tulikuwa tumealikwa pamoja, ghafla mwimbaji mwenzangu Frank Msirikali alinisikia na kuniambia mbona kama unafaa zaidi ukiimba Bass nikacheka tu."anaeleza

*Kutoka Sauti ya Matumaini hadi Sonda ya Dihlu mwaka 2014*
Fabiani anasema siku waliyokutana na Sonda ya Dihlu katika Kanisa la Machimbo alifanikiwa kuimba Bass, Ndipo mwimbaji wa  solo wa Sonda ya DiHlu kwa wakati ule  Jackson Fanuel akanikaribisha  kwenye mazoezi,aliomba  kujiunga na Sonda ya Dihlu na akakubaliwa kuwa mwimbaji wa sauti ya pili na Bass japo muda mwingine inapobidi huwa anaimba kidogo sauti ya kwanza.

*Jina Mr. BASS *
"Mwaka 2017 nikiwa  chuoni pamoja na roommate wangu Salim, nilimuomba ani rekodi clip fupi ninayoweza kuweka mtandaoni, alifanya hivo na mwishoni kama utani akasema "hebu hakikisha kazi yako kwanza Mr. BASS kabla sijaondoka"anasema

"hafla wazo likanijia kwanini nisilitumie hili jina kama utambulisho wa kazi zangu, ndipo rasmi nikaanza kufahamika kama Mr. BASS kupitia video clip zisizozidi dk 1 Ikiwemo wimbo wa Turn your Radio on, Swing Low Sweet Chariot na nyinginezo"
"Katika hali isiyotarajia mwaka 2018 mwezi Februari katika mikutano ya Maisha Hatimaye iliyokuwa ikifanyika mkoani Mbeya chini ya ATAPE  ikirushwa mbashara kupitia Hope Channel Tanzania na Morning Star Radio akiwa na Sonda ya Dihlu katika kipindi cha Lulu za injili Mtangazaji aliendesha kipindi hicho Maduhu Emanueli  aliniulizia "Mr.BASS! Kwanini unajiita Mr.BASS" nami nikamjibu "kwa sababu Mungu amenibariki kuwa na Bass"
Hiyo ndo siku ambapo mahojiano hayo  yaliiwafikia watu wengi waliokuwa wakifatilia mahubiri hayo na ndipo jina hili likaongezeka thamani maradufu" anaeleza.

*Mr. BASS Music* 

Anasema mwaka 2018 pia  mwanzoni alipokea ushauri kutoka kwa watu akiwemo Salim, kwamba niache room videos zisizo na ubora  na ajaribu kufanya hii kazi katika ubora,na ndipo alipoingia studio na kurekodi na kuanza kazi kwa slogani ya Mr. BASS MUSIC Series #Mzikimtamunisasa na kuachia nyimbo tatu.

Fabian anaeleza kuwa mkakati wake ni kuimba nyimbo zenye ujumbe wenye matumaini, Faraja, onyo, upendo , burudisho na kutumia karama na sanaa kufikisha ujumbe unazoelekeza katika madili mema na kumuheshimu Mungu
Mtazamo News . Powered by Blogger.