MTANGAZAJI

MABORESHO SHERIA MPYA YA MADINI, MAJENGO NA VAT YAFANYWA NA BUNGE LA TANZANIA


 
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango(Mb) na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Prof. Adelardus L. Kilangi wakijadili jambo baada ya kuwasilishwa kwa Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya  Sheria mbalimbali, bungeni Jijini Dodoma.
(Picha na Josephine Majura, Wizara ya Fedha na Mipango)
Bunge limepitisha Muswada wa Sheria wa Marekebisho ya Sheria mbalimbali Namba mbili ya Mwaka 2019 ambao umelenga kutatua changamoto za za kodi ikiwemokodi ya Majengo, madini na Kodi uya Ongezeko la Thamani (VAT).


Muswada huo uliopelekwa Bungeni kwa Hati ya Dharura ulijadiliwa na kupitishwa ambapo  Wabunge mbalimbali walipata fursa ya kutoa maoni yao.



Akizungumza wakati wa kuwasilisha Muswada huo, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mhe. Prof. Adelardus Kilangi, alisema kuwa marekebisho hayo yameondoa kodi ya zuio (withholding tax) kutoka 5% hadi asilimia sifuri kwenye bei ya kuuzia madini ya aina zote kwa wachimbaji wadogo ili kuwahamasisha wachimbaji hao kuuza madini katika masoko ya madini.


Amesema marekebisho hayo yanalenga kudhibiti upotevu wa mapato ya Serikali na kuhakikisha mapato yanayotokana na biashara ya madini yanakusanywa ipasavyo

Muswada huo umependekeza kutoa msamaha wa Kodi ya Ongezeko la Thamani kwa wachimbaji wadogo wa madini watakaouza madini yao katika masoko ya madini na vituo vya ununuzi wa madini.
Prof. Kilangi alibainisha kuwa Muswada huo pia umependekeza kila kiwanja kitozwe Kodi ya Majengo badala ya kila jengo lililopo ndani ya kiwanja husika kwa maeneo ya Halmashauri za Wilaya.



Sheria zilizopitishwa ni pamoja na Sheria ya Ushuru wa Bidhaa Sura ya 147,   Sheria ya Kodi ya Mapato  Sura ya 332,  Sheria ya Mamlaka za Serikali za Mitaa ya Utozaji wa Kodi ya Majengo Sura ya 289, Sheria ya Madini Sura ya 123 na  Sheria ya Kodi ya Ongezeko la Thamani Sura ya 148.



No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.