MTANGAZAJI

MAKAMU WA KIONGOZI WA KANISA LA WAADVENTISTA WA SABATO ULIMWENGU AELEKEA KAHAMA,SHINYANGA




Makamu wa Kiongozi Mkuu wa Kanisa la Waadventista Ulimwenguni Mchungaji Geofrey Gabriel Mbwana anatarajiwa kuhutubia mamia ya waumini wa Kanisa la Waadventista Wa Sabato mjini Kahama kwenye mkutano wa Makambi ya kanda ya Kahama yaliyoanza leo jioni.

Mchungaji Mbwana anayetokea yalipo makao makuu ya Kanisa la Waadventista Wa Sabato Maryland,Marekani amekuwepo nchini toka juma lililopita alipokuwa akihutu kwenye Makambi ya Musoma Mjini yaliyokuwa yakihudhuriwa na watu wazima wapatao 10,000 na watoto 5,000 yaliyofungwa mjini humo jana.

Makambi ya Kanda ya Kahama ambayo yamepewa Kauli mbiu ya Kuutwaa Ushuhuda wa Shahidi Mwaminifu  yanatarajiwa kurushwa mbashara na Morning Star Radio pamoja na Morning Star Televisheni yatakuwa yakihudumiwa na wachungaji watano wakiwemo Mwenyekiti wa Kanisa la Waadventista Wa Sabato Jimbo Kuu la Kaskazini (NTUC) Dkt Godwin Ole Lekundayo na Mwenyekiti wa Kanisa hilo jimbo la Nyanza Kusini Mchungaji Sadoki Butoke.

Kwaya zinazotarajiwa kuhudumu kwenye Makambi hayo yanayofanyika katika viwanja vya Kanisa la Waadventista Wa Sabato Nyahanga ni  ,Nyasubi,Kahama,Nyahanga Mjini,Majengo,Shunu,Malunga,Igomelo,Mbulu,Buzwagi,Busaka,Mhungula na Mhongolo







No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.