MTANGAZAJI

MAKAMU WA KIONGOZI WA KANISA LA WAADVENTISTA WA SABATO DUNIANI MCH GEOFREY MBWANA AWASILI MUSOMA KWA MAKAMBI


 Image may contain: 5 people, people smiling, people standing and outdoor

 Image may contain: one or more people, people standing, sky and outdoor

Makamu wa Mwenyekiti wa Kanisa La Waadventista Wa Sabato Duniani Mch .Geofrey Mbwana akitoa Marekani yalipo makao makuu ya Kanisa hilo amewasili jana mjini Musoma  katika  uwanja wa ndege Mjini Musoma Mkoani Mara ambapo ni  Mgeni Rasmi na Mnenaji mkuu wa mkutano wa makambi ya mitaa Mitano ya mjini humo.

Mkutano huu unatarajiwa kukusanya zaidi ya waumini elfu 10,000 kutoka katika makanisa mbalimbali ya Waadventista wa Sabato Musoma mjini na nje ya mji huo.

Kiongozi huyo ambaye ni Mtanzania  amepokelewa na Mwenyekiti wa kanisa hilo Jimbo Kuu la Kaskazini mwa Tanzania  Mch, Dkt. Godwin Lekundayo, Mhazini Mkuu Dickson Matiko, Mwenyekiti wa jimbo  la Mara Mch. Ezekiel Ojwan'g,Katibu Mch Enoch Marwa Sando wakiongozwa na  vikosi mbalimbali vya watafuta njia.

Mkutano huu ulioanza Agosti August 13 mwaka huu utahitimishwa Agosti 20 mwaka huu na unafanyika katika viwanja  vya Kanisa la Waadventista wa Sabato Nyamatare.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.