MTANGAZAJI

DAR ES SALAAM:CHAMA CHA WAMILIKI NA WAENDESHA MITANDAO YA KIJAMII KUFANYA MKUTANO WAKE MKUU

-->  
Mwenyekiti wa muda wa Chama cha Wamiliki wa Blog (TBN),Joachim Mushi akizungumza na waandishi wa habari
Ofisa Uhusiano wa NMB,Doris Kilale akikabidhi mfano wa hundi ya shilingi Milioni 10 kwa Mwenyekiti wa muda wa Chama cha Wamiliki wa Blog (TBN),Joachim Mushi kwa ajili ya mkutano mkuu utakaofanyika Desemba 5 hadi 6 jijini Dar es salaam

 Chama cha Wamiliki/Waendeshaji wa Mitandao ya Kijamii nchini 'Tanzania Bloggers Network' (TBN) kitafanya mkutano wake kwa siku mbili kuanzia kesho jijini Dar es salaam ukiwahusisha wanachana wake toka mikoa mbalimbali nchini.

Akitoa taarifa ya mkutano huo iliyoambatana na upokeaji wa hundi ya shilingi milioni 10 toka NMB Mwenyekiti wa muda wa TBN Joachim Mushi amesema lengo la mkutano huo ni wanatasnia kupewa semina juu ya uendeshaji mitandao ya jamii kwa manufaa, upashaji habari kwa kutumia mitandao yao kwa kuziangatia maadili na namna ya kunufaika na mitandao hiyo kwa waendeshaji (kujipatia kipato) hasa ukizingatia kuwa wapo baadhi yetu tunaifanya kama ajira nyingine.
-->

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.