DAR ES SALAAM:RAIS WA TANZANIA AWATAKA WATANZANIA KUONDOA TOFAUTI ZAO NA KUJENGA NCHI
Rais Mteule Dr John Pombe Joseph Magufuli, ameapishwa leo Novemba 5,2015
kuwa rais wa awamu ya tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Rais Magufuli kutoka chama tawala cha CCM, ameapishwa baada
ya kutangazwa mshindi wa uchaguzi mkuu uliofanyika Oktoba 25 mwaka huu ambapo
alipata asilimia 58.46 ya kura zote, akimshinda mpinzani wake wa karibu, Edward
Lowassa aliyepata asilimia 39.97 ya kura.
Sherehe za kuapishwa kwa Dr. Magufuli,zimefanyika kwenye uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam na zimehudhuriwa na
viongozi kutoka nchi mbalimbali Duniani akiwemo Rais wa Zimbabwe, Robert Mugabe, ambaye ni
mwenyekiti wa Umoja wa Afrika ambapo Dr Magufuli amewataka wananchi kwa ujumla
kufuta tofauti zao ili kuijenga Tanzania Mpya.
Kuapishwa kwa rais Magufuli kumeiingiza taifa la Tanzania
katika historia ya kuwa na Makamu wa rais wa kike Mhe Samia Suluhu Hassan kutoka visiwani Zanzibar,tangu taifa
hili kupata uhuru.
Post a Comment