MTANGAZAJI

DAR ES SALAAM:WANAWAKE WANAOUGUA KANSA YA KIZAZI NCHINI TANZANIA KUPATA MATIBABU BURE






Wanawake wanaougua maradhi ya kansa ya kizazi nchini Tanzania  wamepunguziwa adha ya kusumbuka na gharama za matibabu zinazo wakabili.

 Vodacom Foundation kupitia kwa Mkurugenzi wake Renatus Rwehikiza anasema  ugonjwa wa kansa ya kizazi umekuwa tishio nchini Tanzania  na umesababisha vifo vya akinamama wengi na kufikia asilimia 38.4  ukiondoa wagonjwa wa kansa za aina nyingine hivyo taasisi hiyo imetoa kiasi cha dola za Marekani  87,400 kwa ajili ya kuwawezesha kina mama kwa kuwaleta katika taasisi ya uchunguzi na matibabu ya kansa ya Ocean Road kwa ajili ya uchunguzi wa awali na kupatiwa matibabu.
 
Amesema Tanzania pia ni nchi yenye vifo vingi vinavyotokana na  kansa barani Afrika,hivyo lazima magonjwa tishio nchini yatiliwe mkazo ili kutokomeza na kunusuru wananchi kutokana na vifo vinavyotokana na ugonjwa huu.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.