MANYARA:AKAMATWA NA POLISI KWA TUHUMA ZA KUKUTWA NA MENO YA TEMBO
Jeshi la Polisi Mkoani Manyara
linamshikilia Mtu mmoja anayefahamika kwa jina la Lemnyake Mbaile mwenye miaka 63
mkazi wa Kijiji cha Makame Wilayani Kiteto Mkoani Manyara kwa tuhuma za kukutwa
na meno ya tembo.
Kamanda wa Polisi Mkoani Manyara
Kamishna Msaidizi Wa Jeshi La Polisi Christopha Foime amethibitisha kukamatwa
kwa mtuhumiwa huyo ambapo mahojiano baina yake na jeshi la polisi yakikamilika
atafikishwa mahamani kujibu mashtaka yanayomkabili.
Kamanda Foime amesema walipata
taarifa hizo na kuweka mtego kisha walifanikiwa kumkamata huku ikielezwa kuwa
katika kijiji cha Makame ambako mara kwa wamekuwa wakikamata wawindaji haramu wa
wanyama pori.
Nao baadhi ya wananchni Wilayani Kiteto
wameitaka serikali kuboresha mawasiliano ya simu na barabara ili kurahisisha
kutokomeza vitendo vya ujangili na kufikia adhima ya serikali kufanya hivyo.
Post a Comment