MTANGAZAJI

GOMA:TAMASHA LA MIAKA 30 YA INJILI FAMILY CHOIR KUFANYIKA AGOSTI 30,2015




Acacia Singers

Tamasha la kutimiza Miaka 30 ya Injili Family Choir ya huko Goma,DRC iliyoanzishwa mwaka 1985 linafanyika mjini humo kesho Agosti 30,2015  ikiwa ni maalum kwa ajili ya shukrani kwa MUNGU kuingoza kwaya hiyo kwa muda huo ikifanya kazi ya injili na ambayo pia  imefanikiwa kuweko kwa kwaya 150 katika makanisa ya Waadventista Wa Sabato mjini Goma.

Kwa mwaka huu wa 2015 kwaya hiyo imetoa toleo jipya la audio liitwalo Songa Mbele lenye nyimbo 10 huku santuri mwonekano ya tano ikitarajiwa kutoka hivi karibuni 

Waimbaji wa Acacia Singers toka Tanzania wamewasili mjini Goma jana Agosti 28 mwaka huu kushiriki kwenye sherehe ya miaka 30 ya waimbaji hao wanaofundishwa na  Norbert Mosheing.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.