MTANGAZAJI

FAHAMU KILICHOELEZWA KWENYE RIPOTI YA KANISA LA WAADVENTISTA WA SABATO ECD HUKO SAN ANTONIO



 
Baadhi ya mambo yaliyoelezwa kwenye ripoti ya Viongozi wa Kanisa la Waadventista Wa Sabato katika Ukanda wa Afrika Mashariki na Kati kwenye Mkutano Mkuu wa Kanisa hilo unaoendelea huko San Antonio Texas Marekani.  
Kumekuwa na ongezeko la washiriki kwa kipindi cha miaka mitano iliyopita ambapo kwa sasa idadi ni washiriki milioni 3 na makanisa zaidi ya elfu 23 katika eneo hilo linalojumuisha nchi 11.


Kukiwa sasa na Unioni konferensi 3,Unioni misheni 3,konferensi 7,na field 13.

Ongezeko la zaka kwa asilimia 67,huku ikieleza kuwa matoleo hayo toka kwa washiriki yamesaidia kujenga majengo mpya ya ofisi za unioni na konferensi katika eneo hilo ambalo 2/3 ya waumini wake ni vijana chini ya miaka 35.


Kuna shule elfu 2 na vyuo vikuu 12,vituo vya afya 136,hospitali 8 na moja inayojengwa jijini Mwanza ambayo inatarajiwa kufunguliwa hivi karibuni.

Vitabu vya Tumaini kuu vilivyosambazwa ni nakala milioni 8.

1 comment

Unknown said...

namba za confrace na union....ninawasiwas nazo

Mtazamo News . Powered by Blogger.