MTANGAZAJI

IRINGA:305 WABAINIKA NA VVU BAADA YA KUPIMA KWA HIARI


Watu wapatao 305 kati ya watu 4,879 mkoani Iringa waliopima afya zao  kwa hiari katika kipindi cha robo ya kwanza ya Mwaka huu wamebainika kuwa na maambukizi ya virusi vya ukimwi (VVU).
Akizungumza katika kikao cha utekelezaji wa shughuli za Ukimwi Mwenyekiti wa Kamati ya Kudhibiti Ukimwi  ambaye pia ni Naibu Meya wa Manispaa ya Iringa Gervas Ndaki, ametoa taarifa zilizotekelezwa na Kamati hiyo mbele ya Baraza la Madiwani.
Ndaki  amesema kuwa kati ya waliojitokeza kupima na kupata ushauri nasaha, wanaume walikuwa 2,417 na wanawake 2,467 ambapo  kati ya watu 305 waliopima kwa hiari na kukutwa na maambukizi, wanaume walikuwa 124 na wanawake 181.
Naibu meya huyo amedai kuwa  huduma ya kuzuia maambukizi ya vvu/ukimwi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto imezingatiwa huku, wajawazito 1,036 wakijitokeza na kupata ushauri nasaha na kupima wakati ambapo kati yao wajawazito 10 sawa na asilimia moja walikutwa na maambukizi.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.