MTANGAZAJI

MAENDELEO YA AFYA YA RAIS KIKWETE




 

 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete jana, Jumanne Novemba 11, 2014, aliendelea kufanya kazi ndogo ndogo wakati akiendelea na matibabu katika Hospitali ya Johns Hopkins.


Kwa mujibu wa ukurasa wake kwenye mtandao wa kijamii wa facebook na twitter Rais Kikwete ameandika kuwa anaendelea na kazi ndogo ndogo kukiwa na maelezo yaliyoambana na picha inayomwonesha akiandika ujumbe katika kitabu kidogo cha kumbukumbu mbalimbali za kiofisini.


Taarifa ya kurugenzi ya mawasiliano ya Rais iliyotolewa jana jijini Dar es salaam ilieleza kuwa Kikwete alianza kuwasiliana na mamia kwa mamia ya wananchi mbali mbali nchini kujibu ujumbe mfupi wa maandishi (SMS) wa kumpa pole, kumtakia heri na nafuu ya haraka ambao amekuwa anatumiwa na wananchi tokea mwishoni mwa wiki.


Aidha, Rais Kikwete juzi alizungumza kwa simu na uongozi wa juu wa Tanzania kwa mara ya kwanza tokea afanyiwe upasuaji. Rais alizungumza na Makamu wa Rais Mheshimiwa Dkt. Mohamed Gharib Bilal, Rais wa Zanzibar Mheshimiwa Dkt. Ali Mohamed Shein na Waziri Mkuu Mizengo Peter Pinda.


Madaktari wanaondelea kumtibu Rais Kikwete juzi waliondoa bandeji kwenye sehemu ambako alifanyiwa upasuaji wakieleza kuwa hali yake inaendelea vizuri na anapata nafuu kwa kasi

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.