MTANGAZAJI

WAADVENTISTA WA SABATO KUAMUA KAMA WATAWAWEKEA MIKONO YA KICHUNGAJI WANAWAKE JULAI MWAKANI


Kanisa la la Waadventista Wa Sabato ulimwenguni huenda likaamua kama litapitisha huduma ya kuwawekea mikono ya kichungaji wanawake na kuwatenga rasmi kwa kazi hiyo kwenye  mkutano  wa Halmashauri kuu ya Kanisa hilo Julai mwakani.
Uamuzi huo umetolewa mapema juma hili na halmashauri kuu ya kikao cha mwaka cha  kanisa la Waadventista wa Sabato duniani kilichofanyika yalipo makao makuu ya kanisa hilo nchini Marekani  ambapo kura 243 kati ya kura 287 ziliunga mkono kusitisha suala hilo mpaka kikao cha mwaka 2015
Kumbukumbu za kanisa hilo zinaonesha kuwa suala la kuwawekea mikono ya wanawake limeanza kujadiliwa miaka 130 iliyopita lakini miaka ya sabini ndipo lilipoanza kupamba moto na hasa katika maeneo ambako washiriki wanataka mabadiliko ikiwemo Marekani baadhi ya maeneo ya Ulaya na kusini mwa Pasifiki huku kamati kuu ya uchaguzi ya kanisa hilo ya mwaka 1990 na 1995 ilipendekeza suala hilo na ajenda hiyo haikuwahi kujadiliwa toka wakati huo.
Mkutano wa Halmashauri kuu ya kanisa la waadventista wasabato hufanyika kila baada ya miaka mitano ambapo hukutanisha zaidi ya viongozi 338 wa ngazi za juu za kanisa kutoka divisheni 13 ulimwenguni ,Takribani miaka 2 imepita toka wajumbe kupatiwa muda wa kutafakari kuhusu wanawake kuwawekea mikono ya kichungaji ambapo Oktoba 14 mwakani swala hilo linatarajiwa kuamuliwa kwa kupigiwa kura.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.