MTANGAZAJI

ABOUD JUMBE AMELAZWA KATIKA HOSPITALI YA TAIFA YA MUHIMBILI

 
Rais Mstaafu wa awamu ya pili wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Aboud Jumbe Mwinyi (94), amelazwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili akisumbuliwa na maradhi ya moyo. 
Akizungumza na wanahabari hii leo Ofisa Uhusiano wa Hospitali ya Muhimbili, Doris Ishenga,amesema Jumbe alipokewa hospitalini hapo tangu Oktoba 12, mwaka huu na amelazwa katika Taasisi ya Moyo baada ya kufanyiwa uchunguzi wa kina. 

Amsema kwa mujibu wa taarifa za madaktari za Kitengo cha Moyo hospitalini hapo, baada ya kumfanyia uchunguzi wamebaini Jumbe anasumbuliwa na ugonjwa wa moyo hali inayobabishwa na kuwa na umri mkubwa. 

“Ni kweli Alhaj Jumbe alifikishwa hapa Muhimbili tangu Jumamosi iliyopita na amelazwa katika wodi ya moyo akisumbuliwa na maradhi ya moyo.
 “Unajua ugonjwa huu unawapata zaidi watu wenye umri mkubwa, madaktari wamesema hali yake si mbaya na wala si nzuri sana,” alisema. 

 Jumbe alikuwa Rais wa Zanzibar kuanzia mwaka 1972 hadi 1984 akishika nafasi hiyo baada ya kuuawa kwa aliyekuwa Rais wa Kwanza wa Zanzibar, marehemu Abeid Aman Karume Septemba 5, 1972.
 Alijiuzulu mwaka 1984  nafasi hiyo ilichukuliwa na Ali Hassan Mwinyi mwaka 1984, ambaye baada ya mwaka mmoja alichaguliwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.