MTANGAZAJI

MOROGOGO:MAGARI YATEKWA NA ABIRIA KUPORWA MALI



Watu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi wamefunga barabara ya Morogoro – Iringa katika eneo la njia panda ya kilosa na kisha kuteka magari na kupora mali za abira.

Tukio hilo ambalo lilitokea saa 8:30 usiku wa kuamkia jana, ikiwa ni siku moja baada ya polisi mkoani humo kumtia mbaroni raia mmoja wa Burundi akiwa na vifaa mbali mbali vinavyotumika katika utekaji wa magari.

Kwa mujibu wa baadhi ya watu walioshuhudia tukio hilo wamesema kuwa watekaji walikua wakirusha mawe na kuvunja vioo vya magari yaliyokuwa yamefika katika eneo hilo, kwa mujibu wa dereva wa gari la kampuni ya MCL, Deo Ngangaa amesema kuwa walipofika eneo hilo la tukio walisikia milio ya risasi na mawe yaliyokuwa yakirushwa.

Hata hivyo dereva huyo amesema walipofika njia panda ya kilosa, kando ya barabara walioona magogo na mawe huku magari matatu yakiwa yamepinduka, huku akisema wameshuhudia watu kadhaa wakiwa wameanguka chini akiwemo dereva wa gari lililokuwa likipelekwa Zambia ambaye pia ni raia wa nchi hiyo aliyejeruhiwa kwa kupigwa na mawe.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.