MTANGAZAJI

MMOJA ASHIKILIWA NA POLISI KWA KUJIFANYA MTUMISHI USALAMA WA TAIFA



Mtu mmoja anashikiliwa na Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam kutokana na makosa mbalimbali ya kujifanya ni mtumishi wa Idara ya Usalama wa Taifa. 

Mtu huyo anayejulikana kwa jina la GUNNER SAIMON MEENA, Mkazi wa Kinyerezi Segerea, anatuhumiwa kuwasumbua wafanyabiashara mbalimbali jijini Dar es Salaam kwa kuwasingizia au kuwatuhumu kwamba wanahusika na makosa yenye kuhatarisha usalama.

Kwa muda mrefu Jeshi la Polisi limekuwa likimtafuta mtu huyo kutokana na malalamiko mengi ambayo yamekuwa yakijitokeza na uchunguzi unaonyesha kwamba jina lake halipo katika orodha ya watumishi wa Idara ya Usalama wa Taifa.

Tukio la mwisho lililomfanya akamatwe ni pale alipomtishia mfanyabiashara mwenye asili ya kisomali aitwaye ABDI MOHAMED DALMAR. 

Katika tukio hilo la kutishia, mtuhumiwa huyo GUNNER SAIMON MEENA ambaye ni Afisa Usalama feki, alidai apatiwe kiasi cha fedha za kitanzania (SHILINGI MILLIONI ISHIRINI NA TANO) ama sivyo angemchukulia hatua mlalamikaji chini ya sheria ya Usalama wa Taifa.

Mlalamikaji alitoa taarifa na ndipo mtuhumiwa akakamatwa katika mtego wa Polsi, Uchunguzi zaidi wa shauri hili unafanyika na mtuhumiwa atafikishwa mahakamani baada ya jalada la kesi yake kupitiwa na mwanasheria wa Serikali.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.