ARUSHA:WANANCHI WATISHIA KUCHOMA KIWANDA CHA VYANDARUA KWA SABABU YA UHARIBIFU WA MAZINGIRA
Zaidi ya wananchi 3000 katika kata
ya Matevesi jijini
Arusha wameandamana na kutishia kuchoma moto kiwanda cha kutengeneza vyandarua cha A TO Z kinachomilikiwa na raia wa kiasia kilichopo Kisongo jijini Arusha,kutokana na madai ya kutiririsha maji machafu yenye kemikali na harufu kali yanayosababisha miguu kubabuka namifugo yao kutozaa takribani miaka mitatu.
Arusha wameandamana na kutishia kuchoma moto kiwanda cha kutengeneza vyandarua cha A TO Z kinachomilikiwa na raia wa kiasia kilichopo Kisongo jijini Arusha,kutokana na madai ya kutiririsha maji machafu yenye kemikali na harufu kali yanayosababisha miguu kubabuka namifugo yao kutozaa takribani miaka mitatu.
Hali hiyo iliyotokea mwishoni mwa
juma lililopita ililazimika askari polisi wenye silaha kufika eneo la tukio baada
ya wananchi hao jamii ya wafugaji kuzingira majengo ya kiwanda wakiwa na silaha
mbalimbali za jadi zikiwemo sime, na fimbo, nakusababisha hali ya
taharuki.
Kwa upande wa afisa mwajili wa A To Z,Godwin Aberd amesema kuwa wameagiza mashine ambazo zitakuwa na uwezo wa kusafisha maji hayo pindi yanapotoka kiwandani ili yaweze kutumika tena kiwandani nakuahidi kutoyaruhusi kutoka nje.
Kwa upande wa afisa mwajili wa A To Z,Godwin Aberd amesema kuwa wameagiza mashine ambazo zitakuwa na uwezo wa kusafisha maji hayo pindi yanapotoka kiwandani ili yaweze kutumika tena kiwandani nakuahidi kutoyaruhusi kutoka nje.
Bw Abed amesema kuwa mashine hizo zimechelewa kufika nchini kutoka nje ya nchi,ila watafanya kila njia kuhakikisha zinachukua muda mfupi kuwafikia ili zianze kutumika mara moja kiwandani hapo na kuondoa changamoto hiyo.
Jeshi la polisi wilayani humo kwa kushirikiana na uongozi wa jiji hilo walifanikisha kutuliza hasira za wananchi hao ambao walikuwa
hawataki kutoka kiwandani hapo
Hata hivyo baada ya majadiliano ya
muda mrefu kwa kuwatumia wazee wa jadi wa eneo hilo zoezi hilo lilifanikiwa kwa
sharti la kutoona maji yakiririka tena
kwenye makazi yao.
Post a Comment