MTANGAZAJI

MARA:WAHUKUMIWA MIAKA MITATU KWA KOSA LA KUWATOROKA POLISI



Mahakama ya Hakimu Mkazi Mfawidhi mkoani Mara imewahukumu kwenda jela miaka mitatu kila mmoja watu wawili baada ya kukutwa na kosa la kuwatoroka askari polisi wakiwa chini ya ulinzi.

Kabla ya huku hiyo kutolewa mahakamni hapo julai 3 mwaka huu,mwendesha mashitaka wa serikali Fransisi Kyela aliiambia mahkama hiyo kuwa juni 30 mwaka huu majira ya saa 5:00 asubuhi watuhumiwa ambao ni Musa Daniel(32)mkazi wa kijiji cha Buhemba wilaya ya Butiama,Machage Marwa (37)mkazi wa kijiji cha Buhemba wilayani Butiama,Maribe Magori (34)mkazi wa kijiji cha Buhemba  na Chacha Mtatiro (28)mkazi wawilaya ya Serengeti.

Watuhumiwa hao wakiwa ndani ya mahakama ya mkoa wakati wakiwa wanakabiliwa na kesi za mauaji kabla ya mahaka kuanza watuhumiwa walipitia dirishani kwa kuruka na kuanza kutimua mbio.

Mwendesha mashitaka wa seriklai aliiambia mhakama kuwa wakati watuhumiwa hao wakiwa katika harakati za kukimbia mtuhumiwa mmoja ambaye alimtaja kwa jina la Machage Marwa alijeruhuliwa kwa kupigwa risasi mbili,sehemu za kiunoni na mguu wa kushoto,hali iliyopelekea kupoteza uhai wakati wakatai akipata matibabu katika hosptali ya mkoa mjini hapa.

Hakimu Richard Maganga aliyekuwa akisiliza kesi hiyo baada ya kuridhishwa na ushahidi uliotolewa na baadhi ya wananchi waliokuwepo mahakamani siku ya tukio,mahakama ilitoa nafasi kwa mwendsha mashitaka wa serikali kutoa pendekezo la aina ya adhabu kwa watuhumiwa.

Mwendesha mashitaka aliiomba mahakama hiyo kutoa adhabu kali kwa watuhumiwa hao ili iwe fundisho kwa watu wengine wenye nia kama hiyo ya kutoroka wakiwa chini ya ulinzi.

Kufuatia ombo la mwendesha mashitaka mahakama hiyo mewahukumu watuhumiwa hao kwenda jela miaka mitatu kila mmkoja huku wakiendelea kukabiliwa kesi ya mauaji waliyokuwa nayo awali.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.