MTANGAZAJI

KANISA LA WAADVENTISTA WASABATO TANZANIA LAFANYA MABADILIKO YA UONGOZI KWA BAADHI YA TAASIS



Kamati kuu ya Union ya Kusini ya kanisa la waadventista wasabato nchini Tanzania , hivi karibuni imefanya mabadiliko ya viongozi na watendaji wa taasisi za kanisa hilo.

Kupitia taarifa iliyotolewa leo kwa wafanyakazi wa Morning Star Radio na Morning Star Televisheni na Mshauri na  mlezi wa Taasisi hizo  Mchungaji Robson Nkoko kwa niaba ya Mwenyekiti  wa Kamati  ya unioni Mchungaji Magulilo Mwakalonge ambaye ndiye mwenyekiti wa Kanisa la Waadventista Wasabato katika Union hiyo, imemteua Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Unioni hiyo Mchungaji Robson Nkoko  kusimamia utendaji wa vyombo vya habari vya kanisa hilo. 

Na aliyekuwa Mkurugenzi wa Taasisi ya Vyombo vya Habari vya Kanisa hilo, Mchungaji Musa Mika ameitwa kufanya kazi ya kufasiri katika kiwanda cha uchapishaji cha kanisa (TAP)  kilichopo mjini Morogoro.

Wakati huo huo aliyekuwa Mhazini wa Tanzania Adventist Press Bwana Mathias Mavanza amechaguliwa kushika nafasi ya aliyekuwa Mhazini wa  Taasisi ya Vyombo vya Habari  vya Kanisa la Waadventista Wa Sabato Tanzania, Koheleth Manumbu, ambaye ameitwa kuwa Mhasibu wa Kitengo cha Huduma ya Nyumbani, Elimu na Maisha Bora (HHES) kilichopo  Morogoro.

Kanisa la Waadventista wasabato nchini Tanzania inamiliki Morning Star Radio, Studio ya Redio ya Waadventista Ulimwenguni na Morning Star TV iliyoko katika maandalizi ya kuanza  matangazo.



No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.