MTANGAZAJI

PWANI:WANAUME WASHINDWA KUPIMA VVU



Imefahamika kuwa idadi kubwa ya wanaume walioko katika ndoa Kibaha mkoani Pwani wameshindwa kujitokeza katika zoezi la upimaji wa virusi vya ukimwi(VVU) na badala yake wanategemea majibu ya wake zao.

Akiwasilisha taarifa ya kamati hiyo katika kikao cha kawaida cha baraza la Madiwani wa mji wa Kibaha hivi karibuni Mwenyekiti wa kamati hiyo, Sloom Baghmesh,amesema ni vyema wanaume nao wakabadilika na kujitokeza kwenda kupima afya zao. 

 Baghmesh alibainisha kuwa sababu kubwa inayotolewa na
baadhi ya wanaume hao kushindwa kujitokeza kwenda kupima VVU ni hofu na kuongeza kuwa inaonekana elimu ya kupima kwa hiari haijaeleweka vizuri kwa kundi hilo.

Kamati hiyo imekuwa ikitembelea vituo mbalimbali vya
afya na kuelezewa changamoto  ambayo inakwamisha jitihada za mapambano dhidi ya ugonjwa huo.Kwa mujibu wa taarifa hiyo kati ya Januari hadi Machi mwaka huu, jumla ya watu 2,746 wakiwamo wanaume 1,003 walijitokeza kupatiwa ushauri na kupima afya zao.

Hata hivyo  kati ya watu waliojitokeza 303 walikutwa na VVU
wakiwamo wanawake 217 na wanaume 86.Utafiti unaonesha kuwa miongoni mwa vichocheo vya maambukizi ya VVU ni majumba ya video,picha chafu za ngono,unywaji wa pombe,kutetereka kwa ndoa,mila potofu na tabia ya kufunga ndoa bila kupima.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.