MTANGAZAJI

KWAYA YA KIJENGE SDA KUANZISHA MRADI WA DUKA NA UNUNUZI WA BUS

Kijenge SDA Choir wakiimba

Zaidi ya shilingi milioni mia mbili zinatarajiwa kukusanywa kati ya mwezi wa nne na wa tano kwa ajili ya kuanzisha mradi wa duka la bidhaa mbalimbali na gari la kwaya ya Waadventista Wa Sabato Kijenge ifikapo disemba mwaka huu.

Miradi hiyo ambayo wadau wake wakuu ni kwaya ya waadventista wasabato kijenge unatarajiwa kuwanufaisha wapenzi wa nyimbo za injili hususan za waadventista wasabato kwa kuwa moja kati ya shughuli zitakazofanyika katika duka hilo ni pamoja na kudurufu nyimbo za kwaya mbalimbali kimkataba na kuziuza.


Akizungumza mapema jana na mwandishi wa habari hii, mkuu wa miradi wa Kwaya ya Kijenge Bi Nelly Mzava ameeleza kuwa bus hilo litakaponunuliwa litatumika kwa ajili ya safari za kwaya hiyo ambayo hufanya uinjilisti ndani na nje ya nchi ya Tanzania.


Fedha hizo zina tarajiwa kupatikana kutoka kwa kanisa,mradi wa nyimbo zitakazokuwa kwenye cd na dvd, pamoja na wafadhili mbalimbali nchini Tanzania watakaoshirikishwa.

Na Abel Kinyongo

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.