MTANGAZAJI

WAUMINI NA VIONGOZI WA DINI WAPINGA MSWADA WA BUNGE

 


Wakristo na viongozi  wa Dini mbalimbali wameungana kupinga Mswada wa Uhamiaji Haramu unaoendelea hivi sasa Bungeni nchini Uingereza,Uzinduzi wa kampeni hiyo unaenda sambamba na Juma la Maadhimisho ya Wakimbizi.

Kampeni hiyo inaungwa mkono na  Askofu wa Chelmsford, Dkt Guli Francis-Dehqani, ambaye aliwasili Uingereza akiwa na umri wa miaka 14 akiwa  mkimbizi kutoka Iran wakati huo.

Anasema, "Muswada huu ungeruhusu Uingereza kuwapa kisogo watu walio katika uhitaji mkubwa - kunyima usalama kwa wale walio katika mazingira magumu. Badala yake utawafungia watu ambao wamekimbia mazingira ya kutisha kwa kuhofia maisha yao.

“Nilifika katika nchi hii nikiwa na umri wa miaka 14 na kupewa ulinzi na kukaribishwa Lakini mapendekezo katika mswada huu yanamaanisha kuwaweka kizuizini watoto wanaohitaji usaidizi gerezani’anaeleza

Mswada wa Uhamiaji Haramu ungezuia watu wanaofika kwa boti ndogo katika nchi hiyo kudai hifadhi. Pia ingeruhusu watu, wakiwemo watoto, kuzuiliwa kwa muda usio na kikomo.

Mapendekezo hayo yamekosolewa na Umoja wa Mataifa, ambayo ilisema "itafikia kupigwa marufuku kwa hifadhi".

Katika video inayoonyesha upinzani wao wa pamoja, viongozi kutoka imani za Kiislamu, Kikristo na Kiyahudi wanasema Mswada wa Uhamiaji Haramu "utawaadhibu" watu wanaotafuta hifadhi kutokana na vita, mateso au ukandamizaji.

Tukiwa watu wa imani, tunajitahidi kumkaribisha mgeni, kumkaribisha, kumpenda, kumlinda, kusikiliza, kujifunza, na kuonyesha huruma. Hivi ndivyo tulivyo," wanasema.



No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.