MTANGAZAJI

MCHUNGAJI WA KIADVENTISTA AKABILIWA NA TUHUMA.

 

Mchungaji wa Kanisa la Waadventista wa Sabato la  Green Bay,Wisconsin Marekani, Cory J. Herthel, amekamatwa na kushtakiwa kwa makosa ya mtandaoni yanayodaiwa kumlenga mtoto nchini Venezuela,kwa mujibu wa taarifa ya  WeAreGreenBay.com

Mashtaka hayo yalitolewa na Ofisi ya Mwanasheria wa Marekani katika Wilaya ya Mashariki ya Wisconsin ni pamoja na kujaribu kutengeneza ponografia ya watoto na kuhamisha nyenzo chafu kwa mtoto mdogo.

Malalamiko hayo yanadai kuwa Mchungaji  huyo mwenye umri wa miaka 40 alikutana na mtoto huyo mara ya kwanza wakati wa kazi yake ya umishonari nchini Venezuela, na hatimaye kudumisha mawasiliano kupitia njia za mtandaoni.

Herthel anadaiwa kuomba video zisizofaa kutoka kwa mtoto huyo kwa kubadilishana na malipo ya pesa, akijitia hatiani zaidi kwa kuripotiwa kumtumia mtoto huyo picha chafu zinazomuonyesha.

Imeelezwa kuwa Mawasiliano ya aina hiyo husababisha kumweka mtoto kwenye madhara makubwa ya kisaikolojia na kihisia.

Konferensi ya  Wisconsin imetoa  taarifa rasmi kuhusu tukio hilo ambayo imeelezaa kuwa "Konferensi ya  Wisconsin ya  Waadventista wa Sabato hivi karibuni imegundua kuhusu madai ya vitendo vya kinyume cha sheria kuhusu Cory Herthel, mchungaji mwenye ajira katika Konferensi hiyo.

Kwa mujibu wa  na sera,Konferensi  Ilijulisha mamlaka husika mara moja kuhusu madai hayo".

Taarifa hiyo inaeleza kuwa Hata kabla ya hitimisho la kisheria la kesi hii, Konferensi ya Wisconsin iliamua kwamba tabia inayohusika ilikuwa ukiukaji mkubwa wa maadili na viwango vya Kanisa la Waadventista wa Sabato. Kwa hiyo ajira ya mchungaji imekatishwa.

Uchunguzi wa kesi hii unafanywa kwa pamoja na ofisi za FBI huko Green Bay na Milwaukee, zikifanya kazi kwa ushirikiano na idara ya polisi ya Green Bay.

Juhudi hizi za pamoja zinalenga kutathmini kwa kina kiwango cha vitendo vya Herthel na kupata ushahidi wote muhimu ili kuithibitisha kesi ya mashtaka.

Iwapo atapatikana na hatia, Herthel anakabiliwa na madhara makubwa ya kisheria. Shtaka la kujaribu kutengeneza ponografia ya watoto hubeba kifungo cha chini cha lazima cha miaka 15, kuongezwa hadi miaka 30 jela kwa sheria za Marekani.

Shtaka linalohusiana na uhamisho wa nyenzo  chafu linaweza kumuongezea miaka kumi jela.

Mbali na muda unaowezekana wa kufungwa jela, kuhukumiwa kwa mashtaka yoyote kutamlazimu Herthel ajiandikishe kama mkosaji wa ngono, na kumtia alama ya kudumu katika kumbukumbu ya umma.




No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.