MTANGAZAJI

TAHADHARI YA DHORUBA JIMBO LA TEXAS

 


Dhoruba nyingine ya msimu wa baridi inatarajia kufunika eneo  kubwa la Kaskazini na Kati ya Texas katika mvua ya baridi na halijoto ya baridi, na kusababisha hali hatari za kusafiri katika sehemu kubwa ya jimbo.

Ofisi za Huduma ya Kitaifa ya Hali (NWS) ya Hewa za Dallas-Fort Worth,Austin na San Antonio zimetoa tahadhari  kuhusu dhoruba ya msimu wa baridi inayohusisha kaunti nyingi kutoka Dallas kaskazini hadi Bexar kusini ambapo imefanya hivyo kwa Houston na Galveston kuhusu kuweko kwa  dhoruba ya majira ya baridi katika  kaunti nyingi kaskazini mwa Houston.

Tahadhari hiyo ilianza kutumika saa 3 asubuhi Jumatatu na itaendelea hadi saa 12 asubuhi Jumatano. "Vipindi kadhaa vya mvua inayoganda na baridi kali kwa siku ya Jumatatu " vilitarajiwa kutokea kwenye  kaunti zilizoathiriwa katika kipindi cha siku mbili imeeleza  NWS.

Kaunti za Burleson, Brazos na Washington kaskazini mwa Houston zilitarajiwa kuona vipindi vya mvua nyepesi inayoganda, na kusababisha mwangaza mwepesi, kwa mujibu wa Ofisi ya NWS ya Houston na Galveston.

Utabiri wa dhoruba ya majira ya baridi ya juma hili  unafuatia  dhoruba kali ya juma lililopita, ambayo ilisababisha uharibifu mkubwa wa miundo kwa nyumba na  maeneo ya biashara,huku ikisababisha kukosekana kwa umeme kwa makumi ya maelfu ya wakaazi  na  kufungwa kwa baadhi ya  barabara kuu katika eneo hilo.



No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.