MTANGAZAJI

TAHADHARI YA DHORUBA YA BARIDI KUENDELEA MAREKANI

 


Theluji zaidi ilianguka huko Buffalo Jumanne hii  baada ya dhoruba ya kihistoria na mbaya ya msimu wa baridi kufunika eneo hilo huku maafisa wa serikali wakihesabu vifo vya siku tatu kufuatia dhoruba mbaya zaidi magharibi mwa New York.

Tayari ukiwa umezidiwa na idadi ya vifo inayoongezeka, kukatika kwa umeme kwa wingi, na marufuku ya kuendesha gari ambayo inatekelezwa na jeshi la Polisi, kumekuwa na ongezeko la theluji ya inchi 2 zaidi magharibi mwa New York hadi Jumanne, Huduma ya Kitaifa ya Hali ya Hewa inasema.

Huu sio mwisho bado,” anasema Mtendaji wa Kaunti ya Buffalo Erie Mark Poloncarz, akiita kimbunga hicho “dhoruba mbaya zaidi pengine katika maisha yetu.”

Mfumoko wa dhoruba, ambao ulianza kabla ya Krismasi, uliipiga Buffalo na theluji ya hadi inchi 49 katika siku za hivi karibuni.

Waliopoteza maisha katika dhoruba ya theluji - mojawapo ya majanga mabaya zaidi yanayohusiana na hali ya hewa katika historia ya eneo hilo - walipatikana katika magari, nyumba na kingo za theluji.

Poloncarz alithibitisha idadi ya vifo vinavyohusiana na dhoruba katika kaunti hiyo kuwa ni 28 katika mkutano na wanahabari Jumanne.

Marufuku ya kuendesha gari ilisalia kutekelezwa katika  jiji la Buffalo kufikia Jumanne, na askari wa jeshi la Ulinzi wa Kitaifa walitumwa kudhibiti idadi ya magari  kwa sababu wakaazi wengi wanapinga  marufuku hiyo, Poloncarz anasema.

Wafanyakazi walikuwa wakisafisha theluji kwenye  barabara ambazo bado zimefungwa ili kuunda njia za magari ya dharura.

Hali nchini humo  haikuwa bora zaidi huku hali mbaya ya msimu wa baridi ikinasa watu katika nyumba kutoka Maine hadi jimbo la Washington na kusababisha kuahirishwa  kwa safari za ndege nyingi, na idadi ya vifo ikiongezeka kote Marekani kwa  zaidi ya 50.

Zaidi ya safari 3,000 za ndege zilisitishwa ndani ama  nje ya Marekani  kwa Jumanne  saa nane mchana kwa saa za Mashariki.




No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.