MTANGAZAJI

DHORUBA YA MAJIRA YA BARIDI YASABABISHA MAAFA MAREKANI

  

Idadi ya vifo kutokana na shambulio la kihistoria la hali ya hewa ya majira ya baridi nchini Marekani ilipanda hadi angalau 50 Jumatatu huku hewa ya baridi ya Arktik  ikiyafanya maeneo mengi ya Marekani kuwa theruji nzito iliyoganda. 

Dhoruba ya majira ya baridi kabla ya Krismasi ilisababisha vifo vya takribani watu 27 magharibi mwa New York - moja ya majanga mabaya zaidi yanayohusiana na hali ya hewa katika historia ya eneo hilo baada ya eneo hilo kukumbwa na theluji ya inchi 43.

Waliofariki wamepatikana kwenye magari yao, nyumba zao na kwenye kingo za theluji. Wengine walikufa walipokuwa wakirusha theluji.Idadi ya vifo nchini kote ilitarajiwa kuongezeka kwani wengi walibaki bila umeme katika hali ya baridi kali na hali mbaya ya barabara inaendelea.

Jiji la Buffalo, New York, imeona baadhi ya uharibifu mbaya zaidi kutoka kwa dhoruba, ikiwa ni pamoja na upepo wa kimbunga na hali ya hewa nyeupe kutoka kwa theluji ambayo iliacha magari ya kukabiliana na dharura yakiwa yamekwama kwenye barabara kuu na barabara za pembeni.

Mtendaji wa Kaunti ya Erie Mark Poloncarz alielezea tufani hiyo kama "dhoruba mbaya zaidi pengine katika maisha yetu" na akaonya kuwa kunaweza kuwa na watu wengine waliokufa. Baadhi ya watu, aliona, walikuwa wamekwama katika magari yao kwa zaidi ya siku mbili.

 Kathy Hochul  ambaye ni Gavana wa New York  mzaliwa wa Buffalo, alisema: "Ni kama kwenda kwenye eneo la vita, na magari yaliyo kando ya barabara yanashtua."

Rais wa Marekani Joe Biden alizungumza kwa simu na Kathy Hochul mnamo Jumatatu, akitoa akiahidi msaada wa serikali kwa jimbo hilo linalopitia uzoefu unaotokana na dhoruba.

Vifo vinne viliripotiwa Canada wakati basi lilipobiringita kwenye barabara yenye barafu karibu na mji wa Merritt, katika jimbo la magharibi la British Columbia.

Kiwango hiki cha dhoruba ya msimu wa baridi hakijawahi kushuhudiwa,kuanzia Canada kusini hadi Rio Grande.

Watabiri wanasema dhoruba itapungua katika siku chache zijazo lakini ushauri umetolewa kuzuia watu kusafiri isipokuwa kwa hali ya dharura.

Dhoruba hiyo imesababisha maafa kwa siku kadhaa lakini huduma ya umeme umerejeshwa baada ya kukatika hapo awali.

Chini ya wateja 200,000 hawakuwa na nishati kufikia Jumapili alasiri. Shirika la Habari la Associated linaripoti.

Maelfu ya safari za ndege zimekatishwa, na kuzuia watu wengi kufikia familia zao wakati wa Krismasi.



No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.