MTANGAZAJI

NUSU TU YA WAKRISTO UINGEREZA WANAWAAMBIA WENGINE IMANI YAO

 


Kushiriki imani ni kipaumbele tu kwa karibu nusu ya Wakristo wa Uingereza, wakati wengi hawajui agizo kuu la  utume wa imani yao, kwa mujibu wa utafiti mpya uliotolewa hii leo.


Katika uchunguzi wa utafiti kwa  Wakristo 2,351 wa Uingereza, ni 49% tu walikubali kwamba ilikuwa muhimu kwa Wakristo kushiriki imani yao na wengine.


Kati ya asilimia 21 waliojitambulisha kuwa Wakristo, wawili kati ya watano (43%) hawakujua lolote kuhusu Agizo Kuu - amri ya Yesu kwa wafuasi wake kwenda kufanya wanafunzi wa mataifa yote.


Hii ilipanda hadi 71% ya watu wazima wanaojitambulisha kuwa Wakristo na robo tatu ya watu wote ambao walisema hawakuwa na ujuzi wa Utume Mkuu.


Vijana (wenye umri wa miaka 18-44) walionesha uwezekano mkubwa wa kujua angalau kidogo kuhusu Utume Mkuu (26%) kuliko wale wenye umri wa miaka 45 au zaidi (14%).


Wale wenye umri wa miaka 18 hadi 44 pia walikuwa na uwezekano mkubwa wa kuwa walihudhuria kanisani katika kipindi cha miezi 12 iliyopita (55%).


Miongoni mwa Wakristo watendaji, 38% walisema kwamba kushiriki imani ya Kikristo na wale ambao hawajui kuhusu hilo ndilo kusudi kuu la kazi ya utume wa kanisa.


Utafiti huo uliofanyika kwa kura ya maoni ilifanywa mtandaoni kati ya Septemba 16 na 18 mwaka huu  2022  ulitekelezwa na kuhamasihwa na Savanta ComRes.


Matokeo haya yametolewa majuma chache baada ya sensa ya mwaka 2021 kufichua kupungua kwa idadi ya watu nchini Uingereza na Wales waliojitambulisha kuwa Wakristo katika muongo mmoja uliopita.



No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.