MTANGAZAJI

WATOTO 981 WAPEWA UJAUZITO WILAYANI KIBONDO

 


Vitendo vya ukatili wa kijinsia kwa watoto vimebainika kukita mizizi katika Wilaya ya Kibondo,Kigoma nchini Tanzania  ambapo ripoti ya Wilaya hiyo inaonesha kuwa watoto 981 wamepewa ujauzito katika kipindi cha miezi sita, Januari mpaka Juni 2021.

Taarifa hiyo imebainika wakati Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Mwanaidi Ali Khamis akiwa wilayani humo kukagua na kujionea utoaji wa huduma za ustawi wa Jamii na masuala ya maendeleo ya jamii.

Naibu Waziri Mwanaidi amesema taarifa hizo haziwezi kufumbiwa macho na badala yake watendaji wanaohusika wafanye kila linalowezekana kuhakikisha watuhumiwa wanapatikana na haki inatendeka katika kipindi kifupi iwezekanavyo.

Naibu Waziri Mwanaidi ameongeza kuwa jamii haiwezi kutegemea miujiza ya mafanikio ya kizazi kijacho endapo itabaki kufumbia macho vitendo vya ukatili wa kijinsia hususani dhidi ya wanawake na watoto kwa kuangalia watoto wao wanapata mimba katika umri mdogo na kukatisha ndoto zao.

 Kuhusu vitendo vya ukatili dhidi ya watoto Naibu Waziri amesema kuwa Sheria ya Mtoto inataja mashauri yao kukamilika ndani ya kipindi cha miezi sita.
Mimba za utotoni ni changamoto kubwa na tishio kwa mustakbali wa wasichana wengi ambao hulazimika kuacha shule na kuwa mama katika umri mdogo na wengine hata kujikuta katika ndoa za utotoni.
Kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa vyote viwili mimba na ndoa za utotoni vinaweka hatarini Maisha ya wasichana

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.