MTANGAZAJI

TAHADHARI YA COVID-19:OBAMA APUNGUZA IDADI YA WAALIKWA SIKU YAKE YA KUZALIWA


 Rais wa 44 wa  Marekani Barack Obama amepunguza idadi ya wageni wanaotarajiwa kuhudhuria sherehe ya maadhimisho ya siku yake ya kuzaliwa mwishoni mwa juma kutokana na tahadhari ya virusi vya Covid-19  ambapo atakuwa anatimiza miaka 60.

Msemaji wa Obama, Hanna Hankins, ameviambia vyombo vya habari kuwa Rais huyo msataafu atapunguza idadi hiyo ikiwa ni tahadhari ya kujikinga na maambukizi ya kirusi cha corona.

"Kutokana na hali ya maambukizi kuongezeka toka juma lililopita familia ya Obama imeamua kulipunguza tukio hilo na hivyo kuhusisha wanafamilia na marafiki wa karibu peke yake"amesema  Hankins.

 "Anashukuru kwa wote wanaomtumia ujumbe wa kheri ya siku yake ya kuzaliwa kutoka mbali na anataraji kuwaona hivi karibuni ."

 Awali ilielezwa kuwa, Obama aliyezaliwa  Agosti 4, 1961 angeongoza sherehe hizo siku ya jumatano katika visiwa vidogo vya  Martha's Vineyard Massachusetts

 Imeelezwa kuwa mamia ya wageni waliokuwa wamealikwa walipaswa kuonesha uthibitisho wa kipimo cha kuonesha kuwa hawana virusi vya Covid-19 kwa ajili ya kuhudhuria tukio hilo na kufuata miongozo ya kujikinga na Corona kwa kufuata taratibu zilizowekwa na mamlaka.

Watu maarufu akiwemo  Oprah Winfrey na  George Clooney, walikuwa wametajwa kuhudhuria .

Afisa wa Ikulu ya Marekani alisema jumanne kuwa Rais wa Marekani Joe Biden hatohudhuria sherehe hiyo,japo anataraji atakutana na Obama hivi karibu na anamkaribisha katika jumuia ya watu wenye miaka 60.

 

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.