MTANGAZAJI

MASHINDANO YA USOMAJI WA BIBLIA KWA VIJANA WA KIADVENTISTA YAFANYIKA HOUSTON MAREKANI

Jumla ya timu 10 za Watafuta Njia kati ya Arobaini toka kwa Makanisa ya Waadvetista wa Sabato katika jiji la Houston,Marekani zimefanikiwa kuingia katika hatua ya pili ya Mashindano ya Uzoefu wa Usomaji wa Biblia yanayoendeshwa na  idara ya huduma za Vijana kwa vilabu vya watafuta njia vya Divisheni ya Kaskazini  mwa Amerika (NAD) mwaka huu.

Hatua hiyo ya kwanza ambayo imefanyika katika Kanisa la Waadventista wa Sabato la Nations of Praise iliwakutanisha watafuta njia 255 kwa kujibu maswali 90 toka katika vitabu vya Ezira,Nehemia,Amosi,Yona,Mika na Hosea ambapo iliwachukua takribani saa 6 kukamilika kwa zoezi hilo na kisha kutangazwa washindi huku Timu tano za Kanisa la Waadventista wa Sabato la Houston International zikiiongoza kwa kushika nafasi ya kwanza kwa kila timu.

Mashindano ya Uzoefu wa Usomaji wa Biblia kwa watafuta Njia yanaendeshwa na NAD ambapo kila timu ya vijana sita wenye umri kati ya miaka 10 hadi 16 husoma Biblia,na kisha kufanya mtihani kutokana na vitabu vya Biblia vilivyopangwa kwa mwaka husika wakiwa chini ya walimu waliopangwa na makanisa mahalia.

Asilimia za upangaji wa matokeo hutokana na majibu ya maswali yaliyoulizwa ambapo timu inayopata asilimia 90 hushika nafasi ya kwanza,asilimia 80 nafasi ya pili na nafasi ya tatu ni iliyopata asilimia 70 ya majibu ya maswali.

Utaratibu wa mashindano ya uzoefu wa Usomaji wa Biblia huanza kwa Mtaa,Konferensi,Unioni na kisha Divisheni na kwa mwaka huu timu za watafuta njia toka kwa makanisa yanayounda Divisheni ya Kaskazini mwa Amerika inayohusisha Marekani na Canada yatahitimisha mashindono hayo huko Salem,Oregon Aprili 17 hadi 18 mwaka huu.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.