MTANGAZAJI

KIJANA MTANZANIA ABUNI MTANDAO WA KIJAMII WA KUWAUNGANISHA WAADVENTISTA DUNIANI




Mtanzania Godlisten Timothy ametengeneza mtandao wa kijamii kwa lengo la kuwaunganisha Waadventista duniani kote unaoitwa SDA Family wwws.sdafamily.com kwa njia ya  kuwasiliana kupitia ujumbe wa papo kwa papo kwa kuonana kamera za vifaa vya kiteknohama,sauti na ujumbe mfupi wa maneno.

Mtandao huo ambao pia unapatikana kwenye  simu janja kwa njia ya Program Tumishi ya SDA Family kwa kuupakua kutoka Google PrayStore unamwezesha mtumiaji kushiriki kwenye mijadala ya Biblia ambapo wahusika wataweza kubadilishana na kutumiana picha,video na nyimbo za Injili ambapo pia kuna Program Tumishi ya Video ambayo ni SDA Videos ambayo inapatikana kupitia Google PlayStore ama kwa tovuti ya www.sdavideos.com  

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.