MTANGAZAJI

TUKUYU: KANISA LA WAADVENTISTA WA SABATO LAVAMIWA NA KUCHIMBULIWA SHIMO KWA MADAI KUNA MADINI

Watu wasiofahamika, wamevamia na kuchimba shimo kubwa ndani ya Kanisa la Waadventista Wa Sabato katika kijiji cha Masoko kilichopo wilayani Rungwe nje kidogo ya mji wa Tukuyu.

 Watu hao inasadikika wanaeneza uvumi kuwa kuna vito au Rupia( pesa ya zamani ya wajerumani). Ofisi ya madini imekanusa kuwepo kwa madini yeyote katika eno hilo huku jeshi la Polisi likiahidi kuwatafuta wote waliohusika na uharibifu huo.

Kanisa hilo ndilo la kwanza katika jimbo la Nyanda za Juu Kusini mwa Tanzania lilijengwa mwaka 1932,jengo la awali lilibomolewa na juu yake kujengwa kanisa jingine mwaka 1967.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.