MTANGAZAJI

DAR ES SALAAM:SERIKALI YAIPONGEZA JUHUDI ZINAZOFANYWA NA TAASISI YA DORIS MOLLEL FOUNDATION ZA KUSAIDIA WATOTO NJITI!


DSC_1839
 Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Saidi Meck Sadiki  akizungumza mbele ya wanahabari, madaktari na baadhi ya akina mama waliokuwa na watoto waliozaliwa kabla ya wakati maarufu kama Njiti (Hawapo pichani). Kushoto ni DoriS Mollel ambaye ni Mwanzilishi na Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Doris Mollel Foundation (DMF) na wengine ni maafisa kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili. (Picha zote na Andrew Chale, Modewjiblog).


 Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imepongeza juhudi binafsi zinazofanywa na Taasisi ya Doris Mollel Foundation (DMF) katika harakati zake za kusaidia watoto wanaozaliwa kabla ya wakati (njiti) na mambo ya elimu hapa nchini huku ikiahidi kuendelea kushirikiana nayo kufikia malengo yake.

Kauli hiyo imetolewa mapema na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Saidi Meck Sadiki  wakati wa kupokea vifaa maalum vya kusaidia watoto njiti vilivyotolewa na taasisi hiyo ya Doris Mollel Foundation  tukio lililofanyika katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili jengo la Watoto.

Mkuu wa Mkoa huyo aliongeza kuwa, Mashirika mengine yaendelee kujitokeza kusaidia huduma za kijamii ikiwemo vifaa kama taasisi ya Doris Mollel kwani  asilimia 100 ya wagonjwa na watu wengine wenye mahitaji katika tiba wanakimbilia Dar es Salaam hasa Hospitali ya Muhimbili.

Hata hivyo kwa upande wake Mwanzilishi na mtendaji Mkuu wa DMF,  Doris Mollel amemweleza Mkuu wa Mkoa Meck Sadik kuwa wataendelea kushirikiana na Serikali bega kwa bega katika juhudi za kusaidia watoto njiti nchini  ikiwemo kutoa elimu, vifaa na usaidizi kwa jamii dhidi ya kukabiliana na watoto njiti nchini.

Katika tukio hilo, Mkuu wa Mkoa  alishudia vifaa hivyo na kupokea kutoka DMF sambamba na kutembelea wodi ya watoto njiti pamoja na ile ya Kangaroo ambayo wamama wenye watoto njiti wanakuwa wanapatiwa uangalizi maalum dhidi ya watoto wao ikiwemo kupata joto la Mama na baadae alipanda mti maalum mbele ya jengo hilo la Watoto kama kumbukumbu na juhudi za wadau katika kusaidia jamii dhidi ya watoto njiti.

DMF imeweza  kusaidia vifaa katika wodi hiyo ya watoto Muhimbili vikiwemo (Suction machines, Oxygen Concentrators na Feeding tubes). Aidha Doris Mollel amebainisha kuwa baada ya hapo wanatarajia kuelekea mikoa ya Kanda ya Ziwa kutoa vifaa kama hivyo huku lengo ikiwa ni kufika mikoa yote ya Tanzania.
DSC_1855
Baadhi ya wafanyakazi wa Hospitali ya Muhimbili wakishuhudia tukio hilo maalum la taasisi ya DMF ilipotoa vifaa hivyo katika kitengo cha Jengo la Watoto.
DSC_1865
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Meck Sadik akipata maelezo juu ya vifaa hivyo vilivyotolewa na Taasisi ya DMF.
DSC_1870


DSC_1929
DSC_1939
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam akimpatia zawadi ambayo ni jozi ya soksi kwa ajili ya kusaidia watoto njiti kwa mmoja wa  wamama waliokuwa katika wodi hiyo ya watoto njiti.
DSC_1873
Keki maalum iliyoandaliwa kwa ajili ya siku maalum ya watoto wanaozaliwa kabla ya wakati maarufu njiti
DSC_1885
Mtoto Amne Salim (3) ambaye ni njiti akikata keki maalum kwa niaba ya watoto wenzake katika tukio hilo mapema leo.
DSC_1891
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam akimlisha keki mtoto Amne Salim katika tukio hilo.
DSC_1897
Mtoto Amne Salim akimlisha keki Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Meck Sadik katika tukio hilo.
DSC_1954
Baadhi ya akina mama waliokwenye mpango maalum wa kutunza watoto wao waliozaliwa njiti ujulikanao kama Kangaroo wakiwa wodini mapema leo wakati wa ugeni wa DMF na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam walipotembelea wodi hiyo.
DSC_1882
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaamm Meck Sadik akipokea na kukabidhi vifaa maalum kwa ajili ya kusaidia watoto njiti katika Hospitali ya Taifa Muhimbili vilivyotolewa na Taasisi ya Doris Mollel Foundation mapema leo.
DSC_1907
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Meck Sadik akipanda mti maalum baada ya zoezi hilo la Taasisi ya Doris Mollel Foundation kutoa misaada ya vifaa vya watoto njiti.
DSC_1912
DSC_1921
DSC_1918

DSC_1900
Mama mzazi wa Doris Mollel akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.