MTANGAZAJI

DAR ES SALAAM:WIZARA YA MALIASILI NA UTALII YAWATAKA WATANZANIA KUTUMIA FURSA ZA UTALII


Adelheim James Meru
Wizara ya Maliasili na Utalii nchini Tanzania imewataka watanzania kutumia fursa za Utalii zilizopo nchini ili kunufaika kiuchumi.


Wito huo umetolewa leo Oktoba 1 jijini Dar es salaam  na Viongozi wa Wizara wakati wa ufunguzi wa  maonesho ya kimataifa ya kukuza biashara ya utalii ya Swahili SITE ambapo wamesema watanzania ni bora wakatumia vyema fursa hiyo ili kukuza pato la taifa kupitia sekta ya utalii
 
Katibu Mkuu wa Wizara ya Utalii nchini humo  Adelhelm James Meru ameeleza mafanikio ya sekta ya utalii kwa asilimia 18 ambapo idadi ya watalii wanaoingia Tanzania kwa kipindi cha mwaka 2014 walikuwa si chini ya milioni moja hivyo amewataka wadau wa sekta ya utalii  nchini  Tanzania kuboresha vituo vya utalii vilivyopo ili kuongeza idadi kubwa ya watalii wanaozidi kutembelea  nchini humo.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.