MTANGAZAJI

DAR ES SALAAM:MASHARTI MAWILI YA KUPIGA KURA WA WALIOPOTEZA VITAMBULISHO VYA KUPIGIA KURA NCHINI TANZANIA HAYA HAPA


http://mtanzania.co.tz/wp-content/uploads/2015/10/Lubuva-PHOTO.jpg
Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Tanzania Jaji Mstaafu Damian Lubuva
Tume ya Taifa ya Uchaguzi nchini Tanzana (NEC) imesema waliopoteza vitambulisho vya kupigia kura wataweza kupiga kura endapo watakuwa na taarifa ya polisi  na majina yao kuwamo katika  daftari la mpiga kura.
Kamishna wa NEC, Mary Stelalongwe ametoa ufafanuzi huo kutokana na kuwepo kwa watu wanaozunguka mitaani kuandika namba za vitambulisho vya wapiga kura na kuongeza kuwa kufanya hivyo ni kosa ingawa amesema  Tume haina  taarifa rasmi ya matukio hayo.
Naye Mwenyekiti wa Tume hiyo Jaji mstaafu Damian Lubuva amesema tume imepeleka taa katika vituo vyote vya kupigia kura   kuepuka kura kuhamishwa na   kuhesabiwa sehemu nyingine hivyo taa hizo zimesambazwa vyote vya kupigia kura ambavyo ni 72,000 nchi nzima.
Akizungumzia  mchango wa vyombo vya habari katika uchaguzi mkuu , Jaji Lubuva ameviomba viisaidie tume kutoa taarifa sahihi ili  uchaguzi uwe wa amani na kuonya kuwa vyombo vya habari havitaruhusiwa kutangaza mshindi wa uchaguzi kabla ya kutangazwa na mamlaka husika ingawa wanaruhusiwa kuripoti matokeo katika  vituo kama yalivyo  

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.