MAURITIUS:SUPERSPORT KWENDA LAIVU ALL AFRICAN GAMES
Meneja
Mkuu wa SuperSport kwa ukanda wa Kusini mwa Afrika, Graeme Murray
akizungumza kwenye mkutano na waandishi wa habari kutoka nchi za Afrika
(hawapo pichani) katika hoteli ya OutriggerHotel & Beach Resort
nchini Mauritius.
SuperSport imetangaza
rasmi kwamba watashika usukani wa kurusha matangazo ya michezo ya 11 ya Afrika Games
kupitia SuperSport 9 Michezo hiyo imeanza juzi.
Kauli
hiyo imetolewa na Mkuu wa uzalishaji wa SuperSport, Alvin Naicker
wakati akizungumza na waandishi wa habari katika mkusanyiko mkubwa wa
MultiChoice uliohusisha waandishi wa habari, masupastaa na chaneli
wanazofanya kazi nazo katika hoteli ya OutriggerHotel & Beach Resort
nchini Mauritius.
Naicker alisema kwa kujiamini kwamba urushaji wa matangazo
hayo ni sehemu ya uuzaji wa sura ya michezo ya Afrika katika mabara
mengine.
Akiwa
katika mazungumzo hayo ambayo yalioongozwa na mmoja wa watu wanaotoa
burudani kubwa ya utangazaji ndani ya SuperSport, Carol Tshabalala
alisema hali hiyo inatokana na uwekezaji mkubwa uliofanywa katika sekta
nzima ya burudani na michezo na kampuni ya MultiChoice.
Mkuu
wa masoko wa SuperSuport, Motheo Matsau akifurahia jambo wakati wa
mkutano na waandishi wa habari katika visiwa vya Mauritius.
Katika
mazungumzo hayo ambapo pia alikuwapo Mkuu wa masoko wa SuperSuport,
Motheo Matsau, Meneja mkuu wa SuperSport kwa ukanda wa Kusini mwa
Afrika, Graeme Murray na mgeni maalum Anthony Baffoe, mchezaji wa
zamani wa kimataifa na Mratibu mkuu wa FIFA na CAF, Naicker alisema
ubora wa chaneli yake unatokana na kuweza kunoa vipaji vya watangazaji
wake kufikia kiwango cha juu kabisa cha ubora.
Kama mwekezaji mkubwa wa masuala ya michezo katika bara la Afrika, SuperSport imepata matokeo ya kuridhisha na yenye tija.
Mchezaji
wa zamani wa kimataifa na Mratibu mkuu wa FIFA na CAF, Anthony Baffoe
akifafanua jambo katika mkutano na waandishi wa habari (hawapo pichani)
Mkuu wa uzalishaji wa SuperSport, Alvin Naicker akisisitiza jambo katika mkutano na waandishi wa habari (hawapo pichani).
Carol Tshabalala wa Supersport akiendesha mkutano na waandishi wa habari.
Post a Comment