MTANGAZAJI

IRINGA:WANANCHI WAILALAMIKIA SERIKALI KUHUSU KERO YA MAJI


Wananchi wa vijiji vya Ilole,kitumbuka,Ilambilole,Ikengeza,Chamdindi  na vingine vilivyopo Katika wilaya ya Kilolo na Ismani mkoani Iringa wameilalamikia serikali kwa kushindwa kutatua kero ya maji iliyodumu kwa muda mrefu katika maeneo hayo.
Wakizungumza kwa huzuni mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa aliyefanya ziara ya kukagua miradi ya maji Katika wilaya hizo Amina Masenza wananchi hao wamesema kumekuwa na ubabaishaji wa kisiasa juu ya namna ya kupelekewa maji jambo ambalo linawafanya waweze kutumia maji yasiyo salama kwa afya zao.
Akijibu kero za wananchi hao Mkuu wa mkoa Amina Masenza amesema kumekuwa na watumishi wa serikali ambao wamepelekwa kusomea utalamu huo lakini bado hawafanyi kazi sawasawa na elimu zao ambapo ameahidi kulishughulikia jimbo hilo pamoja na kusimamia miradi mipya iliyopo ili iweze kuwanufaisha wananchi kwa kupata huduma hiyo kwa urahisi.
Kwa upande wake mhandisi wa Maji na meneja mradi wa Maji vijijini Andrew Kisaru amesema kwasasa wanaongeza nguvu ya udhibiti wa matumizi ya maji kwa kufunga mita kwani kwa sasa Katika jimbo la ismani idadi ya watumiaji inakaribia 15000 ambapo kila kaya inaweza kulipa kiasi cha sh 5000 kwa mwaka ambapo tayari Unit 267 zimefungwa katika maeneo hayo hivyo amewahakikishia wananchi kwa tatizo na kero hiyo ya maji itamalizika kwa wakati muafaka

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.