MTANGAZAJI

DAR ES SALAAM:MABASI YAENDAYO HARAKA YAANZA SAFARI







Mabasi maalumu kwa ajili ya kutoa huduma chini ya mradi wa mabasi yaendayo haraka yameingia nchini tayari kwa kuanza huduma ambapo leo Agosti 17 yamefanya safari Kutoka Ubungo kwenda Kimara na kutoka Kimara hadi kivukoni Bure.

Mbali na kuanza kwa huduma ya mabasi hayo Kampuni ya ubia ya UDART kwa kushirikiana na wakala wa mabasi yaendayo haraka (DART) pia  inaanza leo kuendesha mafunzo kwa madereva kabla ya huduma ya usafiri kuanza rasmi Oktoba. 

Meneja wa Udart, Sabri Mabruk amesema Ujio wa mabasi hayo na kuanza kwa huduma zake, ndiyo mwisho wa daladala za kawaida kati ya Kimara na Kivukoni na kuongeza kuwa kutakuwa na utaratibu wa kulipa gharama za usumbufu kwa wenye mabasi ya daladala na kisha kuwapangia njia nyingine.

Mabruk amesema Baada ya mafunzo ya wiki mbili kwa madereva, mabasi yaliyoko yatatoa huduma kupitia vituo 10 pekee kabla ya Septemba ambayo idadi ya mabasi itakuwa imekamilika.

Mabasi hayo yanayotarajiwa kutumia dakika 20 kutoka Kimara hadi Kivukoni eneo la Magogoni ambapo ndani yana viti kwa ajili ya wazee, wajawazito wenye, ulemavu na mikanda maalumu ya kushika kwa abiria wanaosimama.




No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.