MTANGAZAJI

DAR ES SALAAM:UHAKIKI WA TAARIFA KATIKA DAFTARI LA WAPIGA KURA SASA AGOSTI 18 HADI 22 MWAKA HUU



Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), imesogeza mbele uhakiki wa taarifa za uandikishaji wananchi katika daftari la wapigakura kwa kutumia mfumo wa BVR kwa Mkoa wa Dar es Salaam. 

Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Nec, Ramadhani Kailima  amesema  kuanza uhakiki taarifa za wakazi wa mkoa huo waliojiandikisha katika daftari hilo, utaanza Agosti 18 hadi 22, mwaka huu.

 Wiki iliyopita NEC ilitangaza kuanza kuhakiki kwa taarifa za wapiga kura kwa mkoa huo Agosti 15 hadi 19, mwaka huu.



Kailima amesema hatua hiyo inatokana na changamoto za mifumo ya uchakataji wa taarifa za wapigakura ili kuondoa mapungufu yanayoweza kujitokeza na kuchukua muda wa  kukamilisha uchapaji wa daftari la awali la wapigakura kwa mkoa huo.

Amesema kutokana na changamoto hizo, Tume inawatangazia wakazi wa mkoa huo kuwa daftari hilo litawekwa wazi kwa ajili ya kukaguliwa kuanzia kesho hadi Jumamosi ijayo.




No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.