MTANGAZAJI

ARUSHA:WAFANYABIASHARA WALALAMIKIA TATIZO LA KUKATIKA KWA UMEME




 

Wafanyabiashara mkoa wa Arusha hasa wanaouza barafu, samaki, na nyama wamelalamikia kitendo cha kukatika umeme mara kwa mara kwa muda wa zaidi ya mwezi sasa hali inayosababisha bidhaa zao kuharibika.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti wakazi wa jiji la arusha wamesema kuwa tangu mwishoni mwa mwezi wa 7 tatizo hilo lilianza kujitokeza hadi sasa bila kupatiwa ufumbuzi.

Aidha kutokana na hali hiyo Afisa Uhusiano wa Tanesco mkoa wa Arusha, Fredy Robert, amekiri kuwepo kwa tatizo hilo huku akisema kuwa taizo hilo linatokana na marekebisho yanayofanyika katika maeneo mabalimbali nchini.

Blog hii imeshuhudia keleleza za jenereta katika maeneo mbalimbali jijini humo hasa maeneo ya biashara.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.