MTANGAZAJI

ARUSHA:MTANZANIA ASHINDA TUZO YA UBUNIFU NA KUZAWADIWA SHILINGI MILIONI 77


Dr Askwar Hilonga (kulia) akipokea tuzo.



Dr Askwar Hilonga akionesha jinsi vichujio vya maji vinavyofanya kazi huko Karatu,Tanzania (Picha zote na BBC)

Mshindi wa Tuzo ya Ubunifu iliyotolewa na taasisi ya Uingereza ya uhandisi ya Royal Academy of Engineering Mtanzania  Dr Askwar Hilonga amesema kiasi cha dola 38,000 za kimarekani sawa na shilingi milioni 77 za kitanzania alizotunukiwa atazitumia katika kuendeleza mradi wake wa kusafisha maji hasa katika maeneo ya vijijini.
Akizungumza hii leo baada ya kuwasili toka nchini Afrika ya Kusini Dr Hilonga ambaye ni mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Afrika cha Nelson Mandela cha Sayansi na Teknolojia kilichopo jijini Arusha amesema kupata tuzo hiyo kutaweza kukuza biashara yake  kwa kasi kwani lengo ni kuwafikia watanzania wengi mapema iwezekanavyo  ili kutokomeza magonjwa ya tumbo, kuharisha, Amoeba,madhara ya Fluoride kwenye meno na mifupa kunakosababishwa na maji yasiyo salama.

Dr Askwar Hilonga,aliyeshindanishwa na washiriki 55 toka nchi 15 za bara la Afrika ametengeneza chujio maalum ya maji ambayo inatumia mchanganyiko wa mchanga na teknolojia ya nano inayotumika kuua wadudu na kuondoa chemikali zilizoko kwenye maji.
Kwa sasa teknolojia hiyo imeshaanza kutumika katika maeneo ya   wilaya ya Arumeru na Karatu huku ikitarajiwa kuwasaidia watu wengi barani Afrika wanaosumbuliwa na  magonjwa ya tumbo na hasa watoto chini ya umri wa miaka mitano.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.