MTANGAZAJI

DAR ES SALAAM:HATIMAYE TUZO YA JAMII 2015 YATOA TUZO SABA ZA JAMII

Wawakilishi wa waliopewa tuzo katika picha ya pamoja na mgeni rasmi


Mwenyekiti wa Kampuni ya Tanzania Awards International LTD Ndugu DJ Malegesi akitoa maelezo ya Tuzo ya Jamii 2015
Mkuu wa wilaya ya Ilala Raymondi Mushi akihutubia


Katibu wa Tanzania Awards International LTD Amani Mwaipaja akitoa maelezo ya tuzo

Mkurugenzi wa Push Mobile Fredy Manento
Mkuu wa Wilaya ya Ilala Raymond Mushi akikabidhi Tuzo ya Heshima kwa kitukuu wa Hayati Julius Kambarage Nyerere

Mkuu wa Wilaya ya Ilala Raymond Mushi akikabidhi Tuzo ya Heshima  ya Nelson Mandela kwa Kiongozi wa Mtandao wa Vijana Tanzania

Mwakilishi wa Familia ya Makamba (Kulia) akipokea Tuzo ya Mwanasiasa kijana aliyopewa January Makamba

Mwakilishi toka Chama cha Wananchi -CUF(kulia)akipokea tuzo kwa niaba ya Tume ya haki za binadamu na utawala bora




Angel Magoti akiimba wimbo maalum


Kikundi cha Sanaa cha Tuzo ya Jamii 2015 kilitumbuiza








Viongozi wa Watu wenye albinism wakiwa katika picha na Mgeni Rasmi pamoja na viongozi wa Tanzania Awards Intenational LTD

Kampuni ya Tanzania Awards International Limited ya jijini Dar es salaam imetoa Tuzo saba za Jamii zikiongozwa na tuzo ya Heshima kwa Rais wa awamu ya kwanza wa Tanzania Hayati Julius Nyerere na aliyekuwa Rais wa Afrika ya Kusini hayati Nelson Mandela kwa juhudi na uzalendo waliofanya kipindi cha uongozi wao.

Akizungumza katika hafla ya Tuzo ya Jamii iliyofanyika Aprili 13,mwaka huu katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es salaam, Mkuu wa wilaya ya Ilala Raymondi Mushi ameipongeza Kampuni hiyo kwa kutoa tuzo hizo katika Jamii na kusema kuwa zinachochea uongozi bora katika Jamii na uwajibikaji.


Mushi Amesema kila mwananchi anapaswa kuwa kiongozi bora kwa mwenzake ili kuiga mifano ya viongozi hao wa zamani ambao waliitumikia nchi na kuacha historia ambazo mpaka leo zinawakumbusha viongozi kutumikia nchi na kuwa wazalendo.


Licha ya tuzo mbili zilizo kwenda kwa waasisi wa Taifa la Tanzania na Afrika ya Kusini,tuzo nyingine  imetolewa kwa Dkt Regnald Mengi kama mtu mwenye mchango mkubwa kwa Jamii,Ndugu Otieno Igogo mlipa kodi bora,Tume ya haki za binadamu na utawala bora,January Makamba mwanasiasa kijana na Mwanasiasa Mtu mzima kwa Profesa Sospiter Muhongo waziri mstaafu wa Wizara ya nishati na madini.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.