MTANGAZAJI

DAR ES SALAAM:MATOKEO YA MTIHANI WA DARASA LA SABA NCHINI TANZANIA MWAKA 2014 YAMETANGAZWA








Baraza La Mitihani Tanzania limetoa taarifa ya matokeo ya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi  uliofanyika Septemba 10 hadi 11 mwaka huu.

Akizungumza na waandishi habari leo  jijini Dar es salaam  Katibu Mtendaji  wa Baraza la Mitihani la Tanzania Dr Charles E. Msonde  amesema jumla ya watahiniwa  808,085 wa shule za msingi  waliosajiliwa kufanya mtihani huo  waliofanya ni watahiniwa 792,122  waliofaulu ni watahiniwa 451,392  sawa na asilimia 56.99 kati ya hao wasichana ni 226,483 na wavulana ni 224,909.

Dr Msonde  amesema takwimu za matokeo zinaonesha kuwa ufaulu katika matokeo yote umepanda  ikilinganishwa na mwaka 2013. watahiniwa wamefaulu zaidi katika somo la kiswahili ambapo ufaulu ni asilimia 69.70 na somo walilofaulu kwa kiwango cha chini ni hisabati lenye ufaulu wa aslimia 37.56.

Baraza la mitihani la Tanzania limefuta matokeo yote ya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi  mwaka 2014 ya mtahiniwa mmoja  aliyebainika kufanya udanganyifu katika mtihani huo na kusema kuwa idadi ni ndogo ikilinganishwa na watahiniwa 13 walifutiwa matokeo mwaka 2013.

Msonde amesema matokeo hayo yamewekwa kwenye  tovuti za baraza la mitihani, wizara ya elimu na mafunzo na ofisi ya waziri mkuu tamisemi ili kila mtahiniwa aweze kuona matokeo yake.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.