MTANGAZAJI

UKEREWE:WAADVENTISTA WA SABATO WAFANYA USAFI WA MAZINGIRA KATIKA MJI WA NANSIO HII LEO



Washiriki wa Kanisa la Waadventista Wa Sabato wanaoendesha mkutano wa injili katika mji wa Nansio wilayani Ukerewe leo wamefanya usafi wa mazingira katika mji huo na viunga vyake.

Akizungumza na morning star radio hii leo mkurugenzi wa idara ya vijana ya kanisa la waadventista wasabato union comferensi ya kaskazini mwa Tanzania mchungaji  Elius Kasika anaye endesha mkutano huo kwa kushirikiana na kwaya nane amesema  kuwa tukio hilo la kusafisha mji ni moja ya shughuli zilizopangwa na mkutano huo kwa kuwa leo ni siku ya usafi katika mji huo.

Waimbaji walioko kwenye mkutano huo wanatoka katika kwaya za Miembeni,Bunda mjini,Misongwi,Shinyanga,Kahama Mjini,Baso,Nyashimba na TUCASA-Sauti.

Kasika amesema lengo la utaratibu huo wakufanya usafi wa mazingira nikuonyesha kanisa kuwa ni sehemu ya jamii hivyo inalo wajibu wakushiriki katika shughuli mbalimbali za kijamii ikwemo maswala ya usafi.

Mkutano huo ulioanza julai 3 ukiwa unadhaminiwa na chama cha wanafunzi wanaosoma kwenye vyuo vya kati na vyuo vikuu wa kanisa la waadventista wasabato nchini (TUCASA) kwa kushirikiana na washiriki wa makanisa ya Nansio,mjini kati,Bukonye,Mulezi,Amkoko,Pilimagule,Butoni na Namagubo kwa lengo lakutoa mafundisho ya afya, familia na kiroho.


No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.