MTANGAZAJI

TARIME:WAKAZI WA INANO WAITAKA SERIKALI KUONGEZA WALIMU WA SAYANSI



Wakazi wa  Tarafa ya Inano wilayani Tarime wameitaka serikali kuongeza walimu wa masomo ya sayansi katika shule ya  sekondari ya Manga ili kuweza kuwanusuru wanafunzi walioko katika shule hiyo wasiendelee kupoteza muda wao wa kuhudhuria masoma bila ya walimu wa masomo hayo .

Mkuu wa shule hiyo Victoria Yonas amesema kuwa shule hiyo iliyojengwa kwa nguvu ya wananchi ina upungufu mkubwa wa idadi ya walimu hasa wamasomo ya sayansi licha ya kubahatika kuwa na vitabu vya kutosha kwaajili ya kufundishia na kujifunzia  pamoja na vya rejea.

Shule hiyo inayotakiwa kupewa hadhi ya kuwa nakidato cha tano na sita imekumbwa na tatizo la kutokamilika kwa mabweni na ukosefu wa vyoo .

Kilio hicho kimetolewa wakati  wa ziara ya mbunge wa jimbo la Tarime Nyambari Nyangwine alipokuwa akifanya mkutano katika viwanja vya shule ya sekondari hiyo iliyopo katika kata ya Manga Wilayani Tarime.

Nyangwine amesema kuwa tatizo la upungufu wa walimu wasayansi ni la nchi nzima na serikali inajaribu kuweka kipaumbele kwa walimu wa masomo ya sayansi ili kuwavutia wanaopenda kusoma masomo hayo wapate nafasi za upendeleo kuongeza idadi iliyopo ili kupunguza tatizo hilo.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.