MTANGAZAJI

DAR ES SALAAM:JWTZ KUFANYA KONGAMANO LA MAADHIMISHO YA MIAKA 50



Jeshi la Ulinzi la wananchi wa Tanzania(JWTZ)  limeeleza kuwa linatarajia kufanya kongamano kubwa  la Kijeshi linalokwenda sanjari na maonyesho ya Zana za kijeshi Jijini Dar es salaam ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 50 tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam,Mkuu wa  Jeshi la Nchi kavu,Meja Jeneral Mustafa Kejuu,Ameeleza kuwa kongamano hilo litafanyika Julai 14 hadi 16 katika  ukumbi wa Mkutano wa Mlimani City.

Ameeleza maonyesho hayo Yatatoa Fursa kwa Washiriki toka Kada Mbalimbali kubadilishana mawazo,kuona na Kutangaza Biashara ya zana za kijeshi.

Aidha Ameeleza kuwa Majeshi Yatakutana Kujadili Namna ya Kukabiliana na changamoto za sasa Za ulinzi Na Usalama wa Dunia Hususani Eneo la Afrika Mashariki ambalo linakabiliwa na changamoto mbalimbali Ikiwemo Uvuvi haramu Uharamia na Jinsi Ya kulinda Maliasili Za Taifa.

Kongamano Hilo litaleta Wajumbe kutoka SADC,Umoja wa Afrika na jumuiya Nyingine za Kimataifa kujadili na kutatua changamoto mbalimbali za ulinzi na usalama na kuweka Mikakati Ya Pamoja kuimarisha Ulinzi na usalama Duniani.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.